SectionsExitSiri Ya Moyo Wangu

Siri Ya Moyo Wangu

Ordinary Time,MarianExit
Chorus

{Siri ya moyo wangu, ni kilio changu

Na kilio cha moyo wangu, niione huruma yako } *2

Mungu wangu kinga yangu, nakuita Bwana

Ukinigeuka wewe nimekwisha mimi

Wewe ndiwe fimbo yangu, kimbilio langu

Ndiwe boma la wokovu, msaada wangu

Niepushie makucha ya dunia

Verse 2

Kikombe cha uchungu nimekunywa kwa harakwa

Sasa kimenikwama

Nimenaswa nimefikwa yamenikuta mimi

Ee Bwana ninakuita mimi ee Mungu njoo unikamilishe

Verse 3

Najua haina thamani, sala yangu ni chafu

Ibada haifai

Nimkimbilie nani zaidi yako wewe

Naililia huruma yako, mkono wako nishike Bwana

Verse 4

Mimi sistahili kabisa kupokea neema

Kutoka kwako Bwana

Ni mchafu ni mdhambi, nimeoza moyoni

Mikono nakuinulia Bwana, machozi yangu nafukia mimi