Chorus
{Simulia sifa zake Mungu
Tangaza maajabu ya Mungu
Kwa viumbe vyote vya dunia} *2n{(Jama) Kweli Mungu ni mkuu
A-tawala mataifa kwa haki yeye kila analolitenda
Kwe-tu ni mapenzi yake Mwenyewe }*2
Verse 2
Tazama dunia ilivyoumbika inavyopendeza
Milima, mabonde, misitu, mito, maziwa na bahari
Mungu ameviumba vyote, hakika vinapendeza
Simulia sifa za Mungu, Mungu wetu wa ajabu
Verse 3
Tazama dunia ilivyoumbika inavyopendeza
Wanyama na ndege samaki wadudu na viumbe vyote
Mungu ameviumba vyote, hakika vinapendeza
Simulia sifa za Mungu, Mungu wetu wa ajabu
Verse 4
Tazama dunia ilivyoumbika inavyopendeza
Katuumba sisi wanadamu kwa sura na mfano wake
Mungu ameviumba vyote, hakika vinapendeza
Simulia sifa za Mungu, Mungu wetu wa ajabun