SectionsExitSimba Wa Israeli

Simba Wa Israeli

Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,MarianExit
Chorus

{ Simba wa Israeli anaunguruma,

Mbingu za shangwe zinatikisika, zinarukaruka

Ulimwengu wa burudani unatetemeka

Miamba mikubwa mikubwa inasambaratika } *2n{n/s/

Ni shangwe na vigelegele, nderemo chereko vifijo, kwa makofi

Shangilieni, Bwana yesu amefufuka

Manowari ya ukombozi imetia nangann/a/

Ni shangwe na vigelegele, ni nderemo na vifijo makofi ya shangwe

Kwa furaha Mwana wa Mungu amefufuka

Manowari ya ukombozi imetia nangann/t/

Ni shangwe, vigelegele, nderemo na vifijo

Waumini pigeni makofi, Mfalme Yesu amefufuka

Manowari ya ukombozi imetia nangann/b/

Ni shangwe na vigelegele, nderemo chereko vifijonshangwe shangwe, ukombozi Kristu Yesu amefufukanya ukombozi manowari imetia nangann} *2

Verse 2

[a] Aliyekufa mtini bila kosa,n/a/ (akakubali) kuungama na dhambi zetu, amefufuka tumetakasika milelen/s/ akakubali kuyatubu makosa yetu, ameshinda tumetakasika milele

Verse 3

Hatima ya nguvu zote za shetani, (imetangazwa)numeangusha utawala wa mwovu na tumwimbie (wote) aleluya

Verse 4

Utakatifu wa mwanzo, tulioupoteza kwa dhambi

Hii Leo, ameurudishanhesabu ya watoto wa Mungu upya tumerudishiwa

Verse 5

Aliye sadaka ya agano jipya

Amedhihirisha utukufu wake machoni petu

Astahili kutukuzwa kwa sauti kuu