Chorus
Sasa ni wakati mzuri twendeni madhabahuni,
Tukatoe sadaka zetu, tulijenge kanisa la Mungun{ Ewe ndugu yangu mkristu,
Changamka, changamka, peleka sadaka kwa Bwana.
Nenda katoe kwa moyo mweupe
Uzipate baraka za Mungu } *2
Verse 2
Mkristu kutoa sadaka,
Ndio wajibu wa kila mmoja,
Hivyo mkristu kumbuka wajibu,
Nenda katoe sadaka kwa Bwana.
Verse 3
Mwambie Bwana Mungu wako,
Baba pokea nilichokileta,
Hiki ndicho ulichonijalia,
Nakutolea kama shukrani.
Verse 4
Zamani za mababu zetu,
Walipeleka sadaka za nyama,
Nasi wakristu wa leo twendeni,
Tupeleke fedha za mifukoni.