SectionsExitSaa Ya Hukumu

Saa Ya Hukumu

Lent,Wedding,Ordinary Time,Wedding,Wedding,Resurrection,Ordinary Time,Ordinary Time,Pentecostal,Ordinary Time,LentExit
Chorus

Saa ya hukumu yangu imefika,

Na wakati wa kufa kwangu umekaribia

Na kitabu cha kumbukumbu yangu kuwa wazi

Yatakaposomwa matendo niliyotenda

Katika siku za uhai wangu duniani

Ni shimo lenye moto ajabu liko mbele yangu

Ninajua nikitupwa humo uhai kwa heri

Nitakwenda wapi mbona simba wamenizunguka

Ninaangamia Bwana ona ninatapatapa.

Sina msaada Bwana njoo unisaidie

Verse 2

Ona adui zangu, sasa wanashangilia

Hata rafiki zangu pia wamejiunga nao

Wanasubiri kwa hamu waone hukumu yangu

Hata mimi mwenyewe mapigo yananienda mbio

Ninakuungamia Mungu wangu nisamehe makosa yangu

Na ndugu zangu ninaomba radhi nimekosa nimekosa sana

Verse 3

Moto unatisha, ni hatari kila upande

Mwanga umepotea, giza limeshika hatamu

Wanyama wenye njaa ona wanavyofurahia

Na nyoka wenye sumu wanajiandaa kunidaka

Na mimi najua bila wewe nimekwisha Mwokozi wangu

Ee Mungu ninakulilia sikiliza ninavyolalamika

Verse 4

Inuka ee Bwana, ili wote washangae

Nyoosha mkono wako, niokoe ee Mungu wangu

Kwa nguvu zako njoo, ee Bwana sema nitainuka

Hata adui zangu washuhudie huruma yako

Nishike mkono Mungu wangu niokoe naangamia

Ee Bwana mapenzi yako yatimizwe nami nitashukurun