Verse 1
Pasipo makosa Mkombozi wetu,
Katika baraza la wakosefu
Na wote walia asulibiwe,
Aachwe Baraba na Yesu afe
Aachwe Baraba na Yesu afe
Verse 2
Ee Yesu washika msalaba wako,
Na unakubali kufa juu yake
Ee Yesu useme sababu gani,
Ya nini mateso makali hayo?
Ya nini mateso makali hayo?
Verse 3
Ni pendo kwa Baba wa uwinguni,
Ni huruma yangu kwa wakosefu.
Ewe mkristu kumbuka mateso yangu,
Uache makosa, uache dhambi
Uache makosa, uache dhambi