SectionsExitNyota Ya Mashariki

Nyota Ya Mashariki

Pentecostal,Ordinary Time,Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Christmas,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeExit
Verse 1

Kakukirimia, uwe ulivyo,

Atakutumia impendezavyo

Akikuinua, inuka, hivyo,

Ninakuombea heri vilivyo;n

Hakunipa hayo, nikuhitaji,

Kwa niliyo nayo, upate maji,

Na mwisho wa hayo, tuvikwe taji,

Tuingie nayo, wa mbingu mji.

Chorus

{ Nimeiona nyota yako mashariki (nyota yako)

Ninajivuna inavyong'ara rafiki (helelelele)

Naandamana kuja unakotamalaki

Kumsujudia Bwana aliyekupa milki (ho ndugu) } *2

Verse 3

Sirudi kwa njia, yake herode,

Anakuvizia, kila upande,

Wivu unamjia, kakunja, konde,

La kukuzuia juu usipande;n

Ni kama Kaini, mwua Abeli,

Au Raubeni, wa Israeli,

Waliotamani, kuzika, hali,

Ya wadogo duni, wake Jalali!

Verse 4

Ninakuombea, usife moyo,

Maana dunia, si rafikiyo,

Wewe fuatia, za Kristu, nyayo,

Aliyekufia, kwa mizigoyo;n

Wa ulimwenguni, watakufumba,

Wazuri machoni, moyo mwembamba,

Hawatatamani, uitwe, mwamba,

Ni wivu moyoni, unawasomba!