SectionsEntranceNyanyukeni Waumini

Nyanyukeni Waumini

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Chorus

{ Nyanyukeni waumini wote tufanye shangwe

Kwa nderemo, kwa vigelegele na kwa vifijo } *2

Bwana asifiwe (sana) Bwana asifiwe (kweli)

Bwana asifiwe Mwathani aragoshuo

Verse 2

Nikiziangalia mbingu ni kazi ya vidole vyake

Mwezi na nyota za mbinguni ulizoratibisha wewe

Verse 3

Uwezo wake Bwana Mungu haupimiki kwa mizani

Mipango yake kwetu sisi haiwezi kubadilishwa

Verse 4

Alikausha baharí ya Shamu ikawa nchi kavu

Waisraeli wakapita kwa uwezo wa Mungu Baba

Verse 5

Na tupigeni tarumbeta vinubi hata na matari

Tuimbe wimbo wake Musa na ule wa Mwanakondoo

Verse 6

Pazeni sauti zenu kwa shangwe hata na vifijo

Sifa pia na utukufu tumpe Bwana siku zote