SectionsEntranceNyanyukeni Waumini Wote

Nyanyukeni Waumini Wote

Entrance
Chorus

(Nyanyukeni waumini wote tufanye shangwe

Kwa nderemo, kwa vigelegele na kwa vifijo ) *2

Bwana asifiwe (sana) Bwana asifiwe (kweli)

Bwana asifiwe Mwathani aragoshuo

Verse 2

Nikiziangalia mbingu ni kazi ya vidole vyake,

Mwezi na nyota za mbinguni ulizoratibisha wewe.

Verse 3

Uwezo wake Bwana Mungu haupimiki kwa mizani,

Mipango yake kwetu sisi haiwezi kubadilishwa.

Verse 4

Alikausha baharí ya Shamu ikawa nchi kavu,

Waisraeli wakapita kwa uwezo wa Mungu Baba.

Verse 5

Na tupigeni tarumbeta vinubi hata na matari,

Tuimbe wimbo wake Musa na ule wa Mwanakondoo.

Verse 6

Pazeni sauti zenu kwa shangwe hata na vifijo,

Sifa pia na utukufu tumpe Bwana siku zote.