SectionsEntranceNjooni Tumwimbie

Njooni Tumwimbie

Pentecostal,Ordinary Time,Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Chorus

Njooni tumwimbie Bwana wetu - kwa shangwe

Njooni kwa masifu kwa nderemo - tuchezen{Njooni tuabudu, njooni tusujudu

Tupige makofi,

Mbele zake Bwana, Mungu wa ulimwengu } *2

Verse 2

Hekalu lake Bwana Mungu linapendeza,

Nyumbani mwake Bwana mna mengi mazuri

Ninatamani kuingia nyumbani mwake

Nikae naye siku zote nyuani mwake

Nipate heri, mbele za Bwana

Verse 3

Mapema leo ninabisha lango ee Bwana

Nifungulie nipokee nipe faraja

Nimelemewa na mizigo mingi ya dhambi

Nyumbani mwake Bwana ndiko kuna uzima

Uzima tele, na usalama

Verse 4

Twendeni sote kwake Bwana Mungu Mwenyezi

Twendeni kwake tupeleke maombi yetu

Tutoe shukrani zetu kwa Mungu Baba

Tutoe na dhabihu zetu kwake Muumba

Sadaka zetu, azipokee

Verse 5

Uhai wetu unatoka kwake Muumba

Tuimbe sifa zake Mungu siku kwa siku

Tuyatangaze maajabu yake popote

Tuseme Bwana ametenda mambo makuu

Kwa watu wote, milele yote.