Chorus
{ Njooni tuimbe, njoni tucheze
Njooni tufurahi, mbele zake Bwana
Piga makofi, piga vigelegele
Shangilieni Bwana leo asubuhi } *2
Verse 2
Sauti ya kwanza semeni aleluya
Sauti ya pili tumsifu Yesu Kristu
Sauti ya tatu na ile ya nne
Waseme pamoja milele amina
Verse 3
Wamama wote pigeni vigelegele
Wababa wote vinanda vipigwe sana
Pigeni filimbi ngoma na kayamba
Watoto wadogo hoye changamkeni
Verse 4
Mataifa yote njoni mbele za Bwana
Makabila yote simameni tuimbe
Nyanyukeni wote pigeni makofi
Shangwe na nderemo vifijo machezo
Verse 5
Bahari na vitu vyote viijazavyo
Milima mito na miti shangilieni
Ndege wa angani na warukeruke
Wanyama kondeni furahini sana