SectionsEntranceNjooni Tuimbe

Njooni Tuimbe

Pentecostal,Ordinary Time,Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Chorus

{ Njooni tuimbe, njoni tucheze

Njooni tufurahi, mbele zake Bwana

Piga makofi, piga vigelegele

Shangilieni Bwana leo asubuhi } *2

Verse 2

Sauti ya kwanza semeni aleluya

Sauti ya pili tumsifu Yesu Kristu

Sauti ya tatu na ile ya nne

Waseme pamoja milele amina

Verse 3

Wamama wote pigeni vigelegele

Wababa wote vinanda vipigwe sana

Pigeni filimbi ngoma na kayamba

Watoto wadogo hoye changamkeni

Verse 4

Mataifa yote njoni mbele za Bwana

Makabila yote simameni tuimbe

Nyanyukeni wote pigeni makofi

Shangwe na nderemo vifijo machezo

Verse 5

Bahari na vitu vyote viijazavyo

Milima mito na miti shangilieni

Ndege wa angani na warukeruke

Wanyama kondeni furahini sana