SectionsExitNjia Za Mkato

Njia Za Mkato

Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeExit
Verse 1

Haraka hara-ka haina baraka,n(ndugu yangu) ka-wia ufike uendapo salama

Jifunze subi-ra na uvumilivu,n(fanya kazi) usipende kupata vya rahisi vya bure

Haupendi kuchoka - wala kutoa jasho

Wategemea - mali ya ndugu yako

Haupendi kungoja - wala kuulizia

Unafuata - njia za vichochoro!n

Chorus

Njia za mkato ee -

Njia za mkato ee ni hatari sana

Zenye mabonde na maporomoko ee-

Na maporomoko ee ni hatari sana

Hizo za vichochoro ee-

Za vichochoroni ee ni hatari sana

Humo wamejaa na wanyang'anyi ee-

Nao wanyang'anyi ee ni hatari sana jihadhari sana

Verse 3

Mbona unataka mali upesi pasipo kutoa jasho

Vijia vya mkato unavipenda

Unaiba wala rushwa unavuna usikopanda

Majibu ya haraka unayapenda

Verse 4

Mbona unafurahia uzinzi pasipo kufunga ndoa

Vijia vya mkato unavipenda

Unapolemewa na ndoa wamkimbilia mganga

Majibu ya haraka unayapenda

Verse 5

Mbona unapokosea wewe wajitetea kwa uongo

Vijia vya mkato unavipenda

Unapokosana na ndugu wasuluhisha kwa vita

Majibu ya haraka unayapenda