Umekosa nini we Yesu
Kushitakiwa bure kwa pilato
Mwenye kustahili hukumun(Si wewe si wewe Bwana ni sisi) x2
Ole msalaba huo mzito
Apagazwa mwana mpenzi wa Mungu
Mwili waenea mateson(Alipa alipa madhambi yetu) x2
Ona Muumba mbingu na nchi
Yupo chini mzigo wamwelemea
Na mtu kiumbe chake kwa ukalin(Ampiga ampiga bila huruma) x2
Huko njiani we Maria
Waonaje hali ya Mwanao
Ni damu tupu na vidondan(Machozi machozi yamfumba macho) x2
Kwa Simon heri ya kweli
Mimi pia Yesu nisaidie
Kuchukua mzigo wa ukombozin(Kuteswa kuteswa pamoja nawe) x2
Uso wa Yesu malaika
Bethlehemu walikuabudu
Bahati yake Veronican(Kupangusa kupangusa Mfalme wanmbingu) x2
Wakimvuta huku na huku
Wauaji wanamchokesha bure
Chini wamtupa bado kwa nguvun(Aibu aibu yao milele) x2
Wanawake waisraeli
Musilie kwa sababu hiyo
Muwalilie hao kwa dhambin(Upanga upanga ni juu yao) x2
Mwokozi sasa ni ya tatu
Waanguka chini ya msalaba
Katika dhambi za ulegevun(Nijue nijue kutubu hima) x2
Muje malaika wa mbingu
Funikeni mwiliwe kwa huruma
Vidonda vyake na utupun(Askari askari wamemvua) x2
Hapo mkristu ushike moyo
Bwana wako alazwa msalabani
Mara miguu na mikonon(Yafungwa yafungwa kwa misumari) x2
Yesu mpenzi nakuabudu
Msalabani unapohangaika
Nchi yatetemeka kwa hofun(Najua najua linaffa) x2
Mama Maria mtakatifu
Upokee maiti ya mwano
Tumemuua kwa dhambi zetun(Twatubu twatubu kwake na kwako) x2
Pamoja nawe kaburini
Zika dhambi na ubaya wa moyo
Yesu tuwe Wakristu kwelin(Twakupa, twakupa sasa mapendo) x2
Katika Roho yangu, Bwana
Chora mateso niliyokutesa
Nisiyasahau madenin(Na kazi na kazi ya kuokoka) x2