SectionsThanksgivingNingelikuwa Kengele

Ningelikuwa Kengele

Marian,Lent,Ordinary Time,Ordinary TimeThanksgiving
Chorus

Ningelikuwa ni kengele mimi ningelia usikie!

Ningelikuwa ni maua mimi ningechanua chanua

Ili niupambe uso wako ewe Mungu uliyeniumban(Tena mimi) ukanipatia akili na mali ili nikutumikien{ Naona fahari ninapotamka maneno haya,

Ninapotazama kwa jinsi ulivyonipenda mimi kupita upeo } *2

Verse 2

Umetamalaki Mungu (Mungu wangu),

Nikulipe nini Bwana (hakika)

Kila ninapotazama, wanadamu tulivyoumbika

Verse 3

Akili na maarifa (yote hayo)

Umetupatia Mungu (tazama)

Sisi viumbe pekee, utashi nao ukatujaza

Verse 4

Neema zako ni kuu (sana sana)

Kwa wanao wote Baba (hakika),

Mvua yako wainyesha hata kwa viumbe wenye dhambi

Verse 5

Shukurani ninatoa (mimi Bwana),

Kiumbe mnyonge Baba (naomba),

Wabariki mayatima, na wale wasio na uwezo