SectionsEntranceNingekua Na Mabawa

Ningekua Na Mabawa

Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Chorus

Ningekuwa na mabawa, ningeruka hadi mbinguni

Ningekuwa na ufunguo, ningefungua mlango wakon{ Niingie nyumbani mwako, nikuimbie Mungu wangu

Katika makao yako, makao ya milele } *2

Verse 2

Malaika wanakuimbia nyimbo nzuri za furaha.

Makerubi hata maserafi wanasifu jina lako

Verse 3

Ningekuwa mimi ni bahari ningevuma kwa sauti

Ningekuwa mimi ni kengele ningelia usikie

Verse 4

Bwana mimi nitakuimbia siku za maisha yangu

Nitaimba sifa zako Bwana ili watu wasikie

Verse 5

Naamini kwamba siku moja nitafika mbele zako

Natamani sana kuja kwako kwenye raha ya milelen