Chorus
Ningekuwa na mabawa, ningeruka hadi mbinguni
Ningekuwa na ufunguo, ningefungua mlango wakon{ Niingie nyumbani mwako, nikuimbie Mungu wangu
Katika makao yako, makao ya milele } *2
Verse 2
Malaika wanakuimbia nyimbo nzuri za furaha.
Makerubi hata maserafi wanasifu jina lako
Verse 3
Ningekuwa mimi ni bahari ningevuma kwa sauti
Ningekuwa mimi ni kengele ningelia usikie
Verse 4
Bwana mimi nitakuimbia siku za maisha yangu
Nitaimba sifa zako Bwana ili watu wasikie
Verse 5
Naamini kwamba siku moja nitafika mbele zako
Natamani sana kuja kwako kwenye raha ya milelen