SectionsEntranceNinataka Kuingia

Ninataka Kuingia

Marian,LentEntrance
Verse 1

Ninataka kuingia, mjini mwa Mungu

Nitashinda nitakaza mwendo nifike

Nikishikwa na shida, nikichoka njiani

Yesu unaniambia uningojee

Verse 2

Naitwa na Yesu Kristu enzini mwake

Nakimbia kukawia hakuna faida

Wote wachelewao hawatapata taji

Mimi sitaki kingine ila uzima

Verse 3

Elekeza macho yangu mlangoni pako

Niongoze nipe nguvu nikilemewa

Ninapojaribiwa, ninaposingiziwa

Yesu unisaidie nisikuache

Verse 4

Mkono wako unishike nisianguke

Najiona kuwa mnyonge nguvu i kwako

Neno lako ee Yesu linanipa uzima

Nikifika nitaimba umeniponya