Verse 1
Ninakulilia Bwana Mungu, nipe neema zakonili shetani asinishinde, niwe wako milele *2
Verse 2
Uwe ndani yangu siku zote, Baba usiniache
Niwe ndani yako siku zote, niwe wako milele
Verse 3
Haki yako na idumu duniani siku zote
Uangaze roho yangu nikutii daima
Ee Baba unilinde
Verse 4
Ee Baba utazame, dunia yageuka
Ndugu wauana, magonjwa yamezidi
Verse 5
Upendo na haupo, kati ya majirani
Kwa kuwa haya yote, ni mwisho wa dunia
Verse 6
Ee ndugu tukumbuke (kwamba) raha za duniani (ovyo)
Kuna faida gani (kweli) kufuata ulimwengu
Na mwisho tusiishi na Baba Mungu ? *2