SectionsEucharistNinakuabudu Mungu Wangu

Ninakuabudu Mungu Wangu

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEucharist
Verse 1

Ninakuabudu Mungu wangu,

Unayejificha altareni,

Ninakutolea moyo wangu,

Usiofahamu siri yako.

Verse 2

Mafahamu yangu yadanganya,

Yanapokuona na kugusa,

Namsadiki Yesu hadanganyi,

Yeye Mungu Mwana na ukweli

Verse 3

Waficha Umungu msalabani,

Na ubinadamu altareni,

Nami naungama zote mbili,

Kama mwivi yule mwenye toba.

Verse 4

Thomas aligusa majeraha,

Nami nasadiki bila shaka

Ewe Yesu nipe pendo lako,

Tumaini kwako na imani

Verse 5

Umeteswa nini Bwana mwema,

Kwa kunipa mkate wa uzima

Yesu unifiche ndani yako,

Ili nilionje pendo lako

Verse 6

Yesu Pelikane nitazame,

Na kwa damu yako nitakase

Tone moja ndilo linatosha,

Na dunia yote yaokoka

Verse 7

Ndani ya mafumbo Yesu yumo,

Atafunguliwa kwangu lini?

Nikuone Yesu uso wako,

Nishiriki nawe heri yako. Amina.