SectionsThanksgivingNinajiskia Mzuri

Ninajiskia Mzuri

Ordinary Time,Ordinary TimeThanksgiving
Chorus

Ninajisikia mzuri (mimi) na mkamilifu

Ninajisikia mkweli (tena) nisiye na hila

Ninajisikia msafi (mimi) kwa matendo yangu

Ninajisikia ni mwema (tena) nisiye na dhambi

Verse 2

Mbele ya watu najituma, kama mtu mwema

Matendo yangu polepole, ya unyenyekevu

Kumbe huu ni wasifu wangu, wasifu wa nje

Wa ndani mwenendo mbaya wenye sifa mbaya

Verse 3

Kupenda mambo ya uwongo, tena ya uzushi

Daima nayasisitiza, ndiyo kazi yangu

Majirani wakigombana ninasikiliza,

Kumbe chanzo cha yote hayo, hii ni siri yangu

Verse 4

Ninakitumia kioo, ninajing'arisha

Kana kwamba mwuumba wangu alinikosea

Kumbe kwa nje napendeza, kama malaika

Kwa ndani mimi ni shetani, mwenye pembe kali

Verse 5

Hebu tazama moyo wako, ukaubadili

Kimatendo hata mawazo, uwe mtu mwema

Mwenendo mbaya daima unafananishwa

Na kumpepea shetani asichoke kwa kazi