Nimeteuliwa Na Mungu
Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeThanksgiving
Chorus
Nimeteuliwa na Mungu Baba nihubiri kwa kuimba*2n{ Nyimbo zinafundisha, nyimbo zaburudisha,
Nyimbo zinafariji, roho zilizovunjika } *2
Verse 2
Kila niamkapo nitamwimbia Bwana Mungu wangu
Nitaimba nyimbo za kumtukuza aliyeniumba
Verse 3
Mungu Baba Mwenyezi kaniteua mimi nihubiri
Nihubiri kwa nyimbo nyimbo za shangwe nyimbo za Mbinguni
Verse 4
Nafundisha kwa nyimbo naburudisha na ninafariji
Natangaza ufalme wa Mungu Baba kwa njia ya nyimbo
Verse 5
Sifa za Mungu Baba zimo kinywani mwangu siku zote
Mimi nitaziimba sifa za Mungu daima milele