Nimeonja Pendo Lako
Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeThanksgiving
Verse 1
Nimeonja pendo lako, nimejua u mwema
Nitakushukuru nitawainua wote wakusifu wewe
Nitawaongoza vyema waimbe kwa furaha
Nitakushukuru nitawainua wote wakusifu wewe.
Chorus
Ukarimu wako Bwana, na huruma yako wewe
Msamaha wako Bwana, na upole wako (wewe)
Umenitendea wema usiopimika
Nitakushukuru nitawainua wote wakusifu wewe
Verse 3
Kina mama simameni, piga vigelegele
Na kina baba nyanyuka mkapige makofi
Verse 4
Watu wote nesanesa chezeni kwa furaha
Inua mikono juu, mshangilieni Bwana
Verse 5
Watawa washangilie, makasisi waimbe
Walei warukeruke, waseme aleluya
Verse 6
Vitambaa mikononi, vipeperushwe juu
Na vichwa viyumbeyumbe kwa mwendo wa kuringa -
Verse 7
Nitakushukuru mimi, na nyumba yangu yote -
Nitayatangaza haya, maisha yangu yote -