SectionsThanksgivingNimeonja Pendo Lako

Nimeonja Pendo Lako

Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeThanksgiving
Verse 1

Nimeonja pendo lako, nimejua u mwema

Nitakushukuru nitawainua wote wakusifu wewe

Nitawaongoza vyema waimbe kwa furaha

Nitakushukuru nitawainua wote wakusifu wewe.

Chorus

Ukarimu wako Bwana, na huruma yako wewe

Msamaha wako Bwana, na upole wako (wewe)

Umenitendea wema usiopimika

Nitakushukuru nitawainua wote wakusifu wewe

Verse 3

Kina mama simameni, piga vigelegele

Na kina baba nyanyuka mkapige makofi

Verse 4

Watu wote nesanesa chezeni kwa furaha

Inua mikono juu, mshangilieni Bwana

Verse 5

Watawa washangilie, makasisi waimbe

Walei warukeruke, waseme aleluya

Verse 6

Vitambaa mikononi, vipeperushwe juu

Na vichwa viyumbeyumbe kwa mwendo wa kuringa -

Verse 7

Nitakushukuru mimi, na nyumba yangu yote -

Nitayatangaza haya, maisha yangu yote -