SectionsExitNimemaliza

Nimemaliza

Lent,Ordinary TimeExit
Chorus

{ Nimeumaliza mwendo nimeumaliza,

Nimevipiga vita vilivyo vizuri

Nimeumaliza mwendo nimeumaliza,

Imani nimeilinda nimeilinda } * 2

Verse 2

Ninakuamuru mbele ya Mungu mbele ya Yesu

Nenda ukauhubiri ule ujumbenwakati ufaao na wakati usiofaa

Kemea, karipia, onya, himiza

Verse 3

Wafundishe watu wafundishe kwa uvumilivu

Utakuja wakati, ambapo watu,nhawatasikiliza mafundisho ya ukwelinna kisha kufuata tama zao

Verse 4

Watakataa kuisikiliza iliyo kweli,

Watajikusanyia walimu tele

Wanaofundisha lipendezalo sikio lao

Lakini, uwe macho, uvumilien//hitimisho//

Nilipojitetea mara ya kwanza hakuna mtu

Aliyesimama upande wangu, waliniacha

Namuomba Mungu asiwahesabie kosa hilo

Na tena namuomba awasamehe

Lakini Bwana Mungu alisimama pamoja nami

Akanitia nguvu na nikaweza kuutangaza,

Ujumbe usikike kwa watu wa mataifa yote kusudi waokolewenn{ Ooh nimewekewa taji ya uzimanooh oho ambayo Bwana atanivika

Oho oho na wala siyo mimi peke yangunooh ooh ho bali na wote aliowapenda }* 6