Nikupe Nini Mungu Wangu
Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Wedding,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Resurrection,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Resurrection,Ordinary Time,Christmas,Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeOffertory
Chorus
{ Nikupe nini Mungu wangu, nikupe nini we Mwokozi
Nikupe nini Bwana wangu cha kukupendeza } *2
Verse 2
Kila nitakachoshika mbona bado ni kidogo
Fadhili unazotenda kwangu mimi naogopa
Ninakuomba Mwokozi, nifanyie msamaha na unipokee
Mema unayoyatenda, nitafanya nini mimi nikurudishie
Verse 3
Nakutolea mkate toka mmea wa ngano
Nakutolea divai ni tunda la mzabibu
Ninakuomba Mwokozi . . .
Verse 4
Mchana hata siku wewe wanisimamia
Na nikiwa safarini waniepusha ajali
Ninakuomba Mwokozi . . .
Verse 5
Nikiwa na matatizo Bwana wanisaidia
Nikiwa kwenye majonzi Bwana unanifariji
Ninakuomba Mwokozi . . .
Verse 6
Kama njia siioni Bwana unaniongoza
Na hata nikipotea kwako unanirudisha
Nitatoa nini mimi, kitakachokuwa sawa, na fadhili zako
Nitaimba vipi mimi, niyataje mema yote, utendayo kwangu