SectionsOffertoryNikupe Nini Ee Mungu

Nikupe Nini Ee Mungu

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Wedding,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Resurrection,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Resurrection,Ordinary Time,Christmas,Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeOffertory
Verse 1

Nikupe nini ee Mungu cha kukupendeza

Uwezo wangu mdogo Bwana waujua

Pamoja na dhiki inayonisonga

Pokea zawadi yangu hii duni

Verse 2

Nikitazama wenzangu wanakutolea

Zawadi nyingi na nzuri za kukupendeza

Kasoro mimi tu natoa kidogo

Wakati mwingine sitoi kabisa

Verse 3

Maisha yangu ya dhiki Bwana wayajua

Unyonge na udhaifu wangu waujua

Sina kitu mimi cha kukutolea

Lakini pokea nafsi yangu Bwana

Verse 4

Nayakabidhi maisha yangu kwako Bwana

Uniongoze katika njia za uzima

Unisaidie wakati wa shida

Kwani ni wewe tu tumaini langu

Verse 5

Kutoa ndugu ni moyo sio utajiri

Ukimtolea Mungu atakuongeza

Uwasaidie watu maskini

Wasiojiweza utabarikiwa

Verse 6

Ninawasihi wenzangu mliojaliwa

Maisha bora mazuri na ya kuridhisha

Msimsahau Bwana Mungu wenu

Toeni kwa wingi mtabarikiwa.