Verse 1
Ni siku kubwa njooni nyote tushangilieni
Kweli kwa shangwe na tupigeni vigelegele
Twaomba Mungu Baba Awabariki awajalie na watoto
Verse 2
Ni siku kuu ya harusi siku ya furaha
Kwani wawili wamepatana kufunga ndoa
Lindeni ndoa yenu Ili kwa dhiki wala faraja msitengane
Verse 3
Mungu alipomuumba mwanamume Adamu
Akamuumbia mwanamke waishi pamoja
Agano lake Mungu Msilivumje, msilitupe, mhifadhi.
Verse 4
Basi wewe mwanamume umpende mke wako
Umlinde na kumtunza asiwe na upweke
Umlinde siku zote Hadi mwenyezi Mungu atakapoamua
Verse 5
Na wewe mwanamke umpende mume wako tu
Na watoto mtakaojaliwa naye Mungu
Uwatunze kwa wema, na kanisani uwapeleke kwake Mungu