Chorus
Ni kweli amezaliwa Mkombozi wetu Masiha
Malaika wanaimba kwa furaha wakimsifu Bwanan{Na sisi tunafurahia Mkombozi wetu kazaliwa
Na utumwa umetutoka aleluya tushangilie } *2
Verse 2
Kwenye mji wa Daudi Mkombozi kazaliwa
Wote twende tukamwone amelazwa manyasini
Verse 3
Tuna haki kufurahi tumepata Mkombozi
Amekuja tukomboa hivyo wote tufurahi
Verse 4
Utukufu juu Mbinguni, na amani duniani
Kwa watu wote wenye mapenzi mema aleluya
Verse 5
Bwana Yesu kazaliwa, amekuja tukomboa
Katuletea wokovu, hivyo tuimbe aleluya