SectionsEntranceNgoja Nicheze

Ngoja Nicheze

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Wedding,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Wedding,Marian,Ordinary TimeEntrance
Chorus

Tazama mimi ninavyopumua,

Tazama mimi nilivyo na nguvu

Tazama mimi ninavyopumua,

Tazama mimi nilivyo na nguvu

Hizo zote - ni neema bure toka kwa Mungu

Na mimi leo - ngoja nicheze muone,

Nitamsifu ngoja nicheze muone,

Bila kuchoka - ngoja nicheze muone aee

Verse 2

Tazama mimi nakula na kushiba,

Tazama mimi nalala nasinzia

Tazama naamka mimi mwenyewe e,

Tazama tazama ah tazama aa aha

Verse 3

Tazama mimi naweza kuongea,

Tazama mimi naimba bila shida

Tazama naweza kucheza mwenyewe e

Tazama tazama ah tazama aa aha

Verse 4

Nikiugua ona napewa pole,nninapofiwa ndugu mwanifariji

Tazama niwapo na shida wanajaa a

Tazama tazama ah tazama aa aha

Verse 5

Nikikosea huwa nasamehewa,

Nikiudhiwa ndugu mwanitetea

Tazama dhuluma haitaniua a

Tazama tazama ah tazama aa aha

Verse 6

Nikifurahi ndugu washerehekea,

Nikiudhiwa ndugu wasononeka

Tazama ninaishi kati ya watu u

Tazama tazama ah tazama aa aha

Verse 7

Na yote haya najaliwa na Mungu,

Amenipenda upeo wa upendo

Tazama na mimi nitamtukuza a

Tazama tazama ah tazama aa aha