Verse 1
Nimekukosa Bwana, kwa moyo wote ninajuta kweli, kwa moyo wote
Roho yangu ina-yohuzunika ninapokuona ulivyokufa
Chorus
{ Natazama Kalvari (Bwana) ulivyotundikwa mtini (kweli)
Mwili wangu wanyong'onyea ulivyosulibiwa } *2
Verse 3
Tena ni mimi Bwana, ni dhambi zangu ulizozifia, msalabani
Kifo cha aibu, kilikufika makusudi mimi, niokolewe
Verse 4
Kwenye kilima kile, walikusonya wakisema wote, asulibiwe
Kifo chako kwetu ni ukombozi wa mioyo yetu, na roho zetu
Verse 5
Unitulize Bwana, kwa mkono wako kwani ninatubu, makosa yangu
Naanguka kwako kifudifudi, ninaomba toba, kwa moyo wote