SectionsEntranceNatazama Kalvari

Natazama Kalvari

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Verse 1

Nimekukosa Bwana, kwa moyo wote ninajuta kweli, kwa moyo wote

Roho yangu ina-yohuzunika ninapokuona ulivyokufa

Chorus

{ Natazama Kalvari (Bwana) ulivyotundikwa mtini (kweli)

Mwili wangu wanyong'onyea ulivyosulibiwa } *2

Verse 3

Tena ni mimi Bwana, ni dhambi zangu ulizozifia, msalabani

Kifo cha aibu, kilikufika makusudi mimi, niokolewe

Verse 4

Kwenye kilima kile, walikusonya wakisema wote, asulibiwe

Kifo chako kwetu ni ukombozi wa mioyo yetu, na roho zetu

Verse 5

Unitulize Bwana, kwa mkono wako kwani ninatubu, makosa yangu

Naanguka kwako kifudifudi, ninaomba toba, kwa moyo wote