Nashukuru Bwana
Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary TimeThanksgiving
Chorus
Nashukuru Bwana, ee Bwana nashukuru sana
Kwa yote yote, uliyonijalia mimi kiumbe chako,
Niliye mdogo mbele yako
Nitaimba sifa zako ooo milele na milele
Verse 2
Siku zote, Bwana wanipa mkate
Japo kidogo, silali njaa, hata siku moja
Verse 3
Shamba langu, nimepanda nimepata,
Mazao mengi, yapo ghalani, ghalani mwangu
Verse 4
Unanipa, nguvu za kuwashinda
Wanaoniwinda, mwili na roho, wanimalize
Verse 5
Bila wewe, mimi siwezi kitu,
Vitu vyote, nilivyo navyo, nimepata kwako
Verse 6
Wema wako, kwangu mimi mwanao,
Haupimiki, nashukuru Bwana, nashukuru Bwana