SectionsThanksgivingNashukuru Bwana

Nashukuru Bwana

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Ordinary TimeThanksgiving
Chorus

Nashukuru Bwana, ee Bwana nashukuru sana

Kwa yote yote, uliyonijalia mimi kiumbe chako,

Niliye mdogo mbele yako

Nitaimba sifa zako ooo milele na milele

Verse 2

Siku zote, Bwana wanipa mkate

Japo kidogo, silali njaa, hata siku moja

Verse 3

Shamba langu, nimepanda nimepata,

Mazao mengi, yapo ghalani, ghalani mwangu

Verse 4

Unanipa, nguvu za kuwashinda

Wanaoniwinda, mwili na roho, wanimalize

Verse 5

Bila wewe, mimi siwezi kitu,

Vitu vyote, nilivyo navyo, nimepata kwako

Verse 6

Wema wako, kwangu mimi mwanao,

Haupimiki, nashukuru Bwana, nashukuru Bwana