Nakula mwili wa Yesu, nakunywa damu ya Yesu
Naburudika daima, narukaruka na Yesu
Naimba wimbo wa Yesu, nachezacheza na Yesu
Natembea naye Yesu, naenda kwetu Mbinguni
{ Mimi nashangalia, (mimi) mimi naburudika
Yesu ameniponya, kweli nina uzima } *2
Mwalimu wangu ni Yesu, tabibu wangu ni Yesu
Mlinzi wangu ni Yesu, mimi nina usalama
Uhai wangu ni Yesu, mapito yangu ni Yesu,
Naenda na Bwana Yesu, naelekea Mbinguni
Rafiki wangu ni Yesu, jabali wangu ni Yesu
Mshindi wangu ni Yesu, mimi nitashinda vita.
Mpaji wangu ni Yesu , mlishi wangu ni Yesu
Mjali wangu ni Yesu, sina budi kumsifu
Kaeni ndani ya Yesu, kaeni pamoja naye
Na Yesu akae kwenu, mtashinda majaribu
Shikeni maneno yake, jifunzeni kwake Yesu
Yesu atawachukua, awapeleke Mbinguni
Maisha ya duniani, pasipo Yesu ni bure
Uzima wa ulimwengu, bila Yesu ni hapana
Kuleni mwili wa Yesu, kunyweni damu ya Yesu
Onjeni damu ya Mbingu, mtaishi siku zote