SectionsOffertoryNakuja Na Zawadi

Nakuja Na Zawadi

Baptism,MarianOffertory
Verse 1

Naondoka mimi naenda kwa Baba,

Nipeleke hiki nilichokipata,

Japo kidogo, sitaona haya,

Nimeamua, sitarudi nyuma

Chorus

{ Nakuja polepole Baba,

Nakuja na zawadi yangu

Naleta mbele zako ili nitoe shukurani } *2

Verse 3

Natembea mimi mwendo wa madaha,

Nakanyaga chini kwa maringo tele,

Naelekea, altare ya Bwana,

Nimkabidhi, nilichojaliwa.

Verse 4

Nimechangamka ninashangilia,

Napiga kelele kelele za shangwe

Nachezacheza, najongea kwako,

Ee Mungu Baba Nipokee mimi.

Verse 5

Nafsi yangu mimi naileta kwako,

Mkate divai pia ninaleta

Uigeuze, mwili na damuyo,

Chakula chetu, tunaosafiri

Verse 6

Mavuno shambani mimi nimevuna,

Mifukoni fedha nimekabidhiwa,

Mimi ni nani, nisikushukuru,

Baba nasema asante kwa yote.