Verse 1
Naondoka mimi naenda kwa Baba,
Nipeleke hiki nilichokipata,
Japo kidogo, sitaona haya,
Nimeamua, sitarudi nyuma
Chorus
{ Nakuja polepole Baba,
Nakuja na zawadi yangu
Naleta mbele zako ili nitoe shukurani } *2
Verse 3
Natembea mimi mwendo wa madaha,
Nakanyaga chini kwa maringo tele,
Naelekea, altare ya Bwana,
Nimkabidhi, nilichojaliwa.
Verse 4
Nimechangamka ninashangilia,
Napiga kelele kelele za shangwe
Nachezacheza, najongea kwako,
Ee Mungu Baba Nipokee mimi.
Verse 5
Nafsi yangu mimi naileta kwako,
Mkate divai pia ninaleta
Uigeuze, mwili na damuyo,
Chakula chetu, tunaosafiri
Verse 6
Mavuno shambani mimi nimevuna,
Mifukoni fedha nimekabidhiwa,
Mimi ni nani, nisikushukuru,
Baba nasema asante kwa yote.