Chorus
Enyi watumishi wa Bwana sifuni
Lisifuni lisifuni Jina la Bwana
Na ahimidiwe Bwana Mungu
Bwana Mungu kutoka Sayuni
Akaaye Yerusalemu aleluya
Verse 2
Ninyi msimamao nyumbani mwa Bwana
Nyuani mwa nyumba ya Mungu wenu
Msifuni Bwana kwa kuwa yu mwema
Liimbieni jina lake kwa maana lapendeza
Verse 3
Kwa sababu Bwana amejichagulia Yakobo
Na Israeli wawe watu wake hasa
Maana najua mimi ya kuwa Bwana ni mkuu
Na Mungu wetu yu juu ya miungu yote
Verse 4
Enyi mlango wa Israeli mhimidini
Enyi mlango wa Haruni mhimidini
Enyi mlango wa Lawi himidini Bwana
Enyi mnaomcha Bwana mhimidini Bwana