SectionsEntranceNa Ahimidiwe Bwana

Na Ahimidiwe Bwana

Ordinary TimeEntrance
Chorus

Enyi watumishi wa Bwana sifuni

Lisifuni lisifuni Jina la Bwana

Na ahimidiwe Bwana Mungu

Bwana Mungu kutoka Sayuni

Akaaye Yerusalemu aleluya

Verse 2

Ninyi msimamao nyumbani mwa Bwana

Nyuani mwa nyumba ya Mungu wenu

Msifuni Bwana kwa kuwa yu mwema

Liimbieni jina lake kwa maana lapendeza

Verse 3

Kwa sababu Bwana amejichagulia Yakobo

Na Israeli wawe watu wake hasa

Maana najua mimi ya kuwa Bwana ni mkuu

Na Mungu wetu yu juu ya miungu yote

Verse 4

Enyi mlango wa Israeli mhimidini

Enyi mlango wa Haruni mhimidini

Enyi mlango wa Lawi himidini Bwana

Enyi mnaomcha Bwana mhimidini Bwana