Chorus
Mwimbieni Bwana zaburi
Mwimbieni kwa kinubi) *2n{Mwimbieni kwa kinubi na sauti ya zaburi
Mwimbieni kwa panda na sauti ya baragumu (wote)
Shangilieni mbele za mfalme Bwana wa majeshi}
Verse 2
Bahari na ivume na vyote viijazavyo,
Ulimwengu na wote wanaokaa ndani yake
Milima naiimbe kwa furaha mbele za Bwana Mungu
Verse 3
Wanyama wa mwituni na mimea ya kondeni
Upepo na uvume kupeleka habari hizi
Kwa ndege wa angani na viumbe vilivyo baharini
Verse 4
Nikitazama kushoto kulia nyuma na mbele
Nikitazama angani nikitazama ardhini
Kila nionacho kinasimulia utukufu wako
Verse 5
Kwa maana mbingu na dunia ni kazi yako
Jua na mwezi na nyota anga pia nayo mawingu
Ni kazi ya vidole vyako na ujuzi wa mikono yako