SectionsExitMvivu Wewe

Mvivu Wewe

Ordinary TimeExit
Chorus

Mvivu wewe mvivu * 3 mvivu wewe

Hebu watazame wadudu hawa

Hebu watazame sisimizi wewe

Wana adili ya kazi pasipo kusimamiwan(Tazama wanavyojituma (jituma) hawalazimishwi

Tena hawana kiongozi (yeyote) wa kuwapangia)*2n{Ewe mvivu utalala we! we! hatarini

Utaondoka lini katika usingizi wako? }*2

Verse 2

Kwa wenzako kunapokucha, wewe nd'o unalala

Wenzako wanapoamka, wewe wajigeuza

Wenzako wakipanga majukumu, wewe waota ndoto

Wenzako wanapotoka kazini, wewe watupa shuka

Verse 3

Wenzako wanafanya kazi, tena kwa kujituma

Wenzako wanafanya kazi, tena kwa moyo mmoja

Daima wewe wajivuta, tena wingi wa maneno

Hata nazo salamu haziishi, tena sababu mia mia.

Verse 4

Hebu jitazame sasa, umbeya wakutawala,

Tena ukijichunguza, na wizi wakuandama

Wenzako wakifanikiwa, waanza kazi kuwaomba,

Na maisha ya jirani, wewe wayafuatilia

Verse 5

Jiulize utabarikiwa, lini ewe mvivu,

Jiulize utaamka, lini ewe mvivu,

Ukishiba leo huwazi, ya kesho utakula nini

Hakuna lolote ufanyalo bila ya kusimamiwa.