Mungu Yule

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Lent,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeThanksgiving
Chorus

{ Nimemuona yule ninayemtafuta na neema zake

Nimemuona -leo nimemuona Mungu } *2n

Mkononi mwake ana uzima tena ni wa milele

Mkononi mwake ana uzima ninaoutafuta

Na uzima huo anatoa bure kwa walio tayari

Lakini kuna kanuni moja ya kwamba, uwajali watu.

Verse 2

Nimemuona Mungu yu mtupu-u hana nguo

Anatamani mimi niende nikamvishe

Nimemuona Mungu ana njaa hana chakula

Anatamani mimi niende nikamlishe

Nimemuona Mungu ni mgonjwa-a kitandani

Anatamani mimi niende kumtazama

Verse 3

Nimemuona Mungu amefungwa-a gerezani

Anatamani mimi niende kumfariji

Nimemuona Mungu ni mkimbizi mpakani

Anatamani mimi niende kumpokea

Nimemuona Mungu ni yatima hana wazazi

Anatamani mimi niende nikamtunze

Verse 4

Nimemuona Mungu ni mjane hana matunzo

Anatamani mimi niende kumhifadhi

Nimemuona Mungu amefiwa ana majonzi

Anatamani mimi niende kumfariji

Nimemuona Mungu ni kilema na hajiwezi

Anatamani mimi niende kumuinua

Verse 5

Nimemuona Mungu atolewa angali mimba

Anatamani mimi niende kumtetea

Nimemuona Mungu anapigwa kwa makombora

Anatamani mimi niende kusuluhisha

Nimemuona Mungu ni mtumwa ananyanyaswa

Anatamani mimi niende kumtetea