SectionsExitMungu Na Shetani

Mungu Na Shetani

Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Lent,Ordinary TimeExit
Verse 1

Ndugu yangu sikia nasema kwa makini,

Habari hii kuu ya ufalme wa Mungu

Inasikika sana, sasa imeenea,

Lakini sio wengi, wanaoiamini

Chorus

Waimbaji tumeshaimba nyimbo nyingi

Makasisi wamehubiri pande nyingin{ Twasema uokoke, nawe wasema kesho

Inapofika kesho, wasema kesho kutwa

Siku nazo zapita, miaka inapita

Uchague mwenyewe, Mungu au shetani } *2

Verse 3

Ukizipata shida, walaumulaumu,

Ndugu na majirani, wadhani umelogwa

Unaanza ugomvi, wachukia wengine,

Hata bila sababu wawaita wachawi

Verse 4

Waomba mara moja, ukikosa majibu,

Kesho inapofika waenda kwa mganga

Ngoja nikueleze, Mungu hana haraka,

Jifunze vumilia majibu utapata

Verse 5

Jifikirie ndugu, usingoje ya kesho,

Muda ni wako sasa, amua ukubali

Mengi tumeyasema, ilobaki ni kwako,

Uchague mwenyewe, Mungu au shetani