Verse 1
Ndugu yangu sikia nasema kwa makini,
Habari hii kuu ya ufalme wa Mungu
Inasikika sana, sasa imeenea,
Lakini sio wengi, wanaoiamini
Chorus
Waimbaji tumeshaimba nyimbo nyingi
Makasisi wamehubiri pande nyingin{ Twasema uokoke, nawe wasema kesho
Inapofika kesho, wasema kesho kutwa
Siku nazo zapita, miaka inapita
Uchague mwenyewe, Mungu au shetani } *2
Verse 3
Ukizipata shida, walaumulaumu,
Ndugu na majirani, wadhani umelogwa
Unaanza ugomvi, wachukia wengine,
Hata bila sababu wawaita wachawi
Verse 4
Waomba mara moja, ukikosa majibu,
Kesho inapofika waenda kwa mganga
Ngoja nikueleze, Mungu hana haraka,
Jifunze vumilia majibu utapata
Verse 5
Jifikirie ndugu, usingoje ya kesho,
Muda ni wako sasa, amua ukubali
Mengi tumeyasema, ilobaki ni kwako,
Uchague mwenyewe, Mungu au shetani