Mungu Baba Pokea

Ordinary Time,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Lent,Ordinary Time,Ordinary TimePresentation of Gifts
Verse 1

Mungu Baba pokea sadaka yetu leo

Tukutoleayo kwa jina la Mwanao

Ya Abeli na Ibrahimu ilikupendeza

Yetu Baba ipendeze uipokee

Chorus

Ipokee - (ipokee) sadaka yetu

Ndilo fumbo - (ndilo fumbo) la kukupendeza

La Baba na Mwana na Roho Mtakatifu *2

Verse 3

Njooni wote tutoe sadaka yetu leo

Kwa sifa na utukufu wake Mwenyezi

Mkate huu na divai ndivyo mwili wake

Kwa heshima kuu sadaka tumtolee

Verse 4

Ee Mwenyezi tupokee tuwe mali yako

Twakusihi kwa heshima utupokee

Tunakutolea nguvu kazi na mavuno

Kwa huruma yako dhambi tuondolee

Verse 5

Kama mwanzo Mungu Baba a-si-fiwe

Na mwanaye ndiye aliyetukomboa

Roho Mtakatifu ndiye wetu mfariji

Utatu Mtakatifu Mungu mmoja twakiri