Chorus
Mtazame Mkombozi msalabani,
Tazama mikono na miguu, vimefungwa kwa misumari
Mtazame Mkombozi msalabani,
Tazama ubavu wake, ulivyochomwa kwa mkuki
Verse 2
Msilie enyi kila mama, msinililieni mimi
Bali watoto wenu, pia nafsi zenu
Verse 3
Mateso gani haya ee Bwana, unayoteseka Mungu wangu
Lipi baya ee Bwana ulilolitenda
Verse 4
Hatia hiyo wanaiunda, hukumuni wanakuingiza
Nawe hujibu neno, wakubali kufa
Verse 5
Nguvu mwilini zimekutoka, mara ya tatu unaanguka
Teso kubwa ee Bwana, lakusonga sana
Verse 6
Juu msalabani unalia, mateso yamezidi sana
Wasema nina kiu, wanakupa siki