Verse 1
{ Ee Mungu Baba Mwenyezi tuko hapa mbele zako,
Tunakulilia Baba utusikilize } *2
Chorus
Ipokee roho ya mwanao, mpokee mtumishi wako
Mpokee anakuja kwako, mpokee mtumishi wako,
Enyi malaika wa mbinguni, mchukue mpeleke kwa Baba,
Mchukue mpeleke kwa baba
Verse 3
Usiyakumbuke Baba makosa aliyotenda,
Umsamehe makosa ya ujana wake
Verse 4
Fariji roho za wote wanaohuzunika,
Uwape matumaini uwape tulizo
Verse 5
Ee Bwana ungehesabu, makosa ya wanadamu,
Ni nani angesimama mbele yako wewe
Verse 6
Ee Mungu mwenye rehema kumbuka rehema zako
Maana zimekuwapo tokea zamani