SectionsOffertoryMpeni Kaisari

Mpeni Kaisari

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,Wedding,Ordinary Time,Ordinary TimeOffertory
Verse 1

Vipaji tumepewa, mapato tumepata

Lakini binadamu tunashindwa kushukuru

Wakati tunaomba, tunajinyenyekesha

Lakini tukipata mikono yetu birika

Chorus

Mpeni kaisari, yaliyo yake

Mpeni Mungu (yale) yaliyo yake Mungu *2

Verse 3

Mifugo tunafuga, nafaka tunavuna

Lakini kila siku tunakula na kusaza

Kumbuka kuna wale, wasio na chochote

Hawawezi kupata, hata kikombe cha chai

Verse 4

Tunapofanya kazi, twapata mishahara

Shughuli zetu sisi kuingia kwenye baa

Ikiwa zitabaki, twakuja kanisani

Twamtolea Mungu, shilingi moja na tano

Verse 5

Tukiwa na wagonjwa hatuwasaidii

Wakati wamekufa tunachanga kwa huzuni

Twachukua mikopo, kwa mambo ya anasa

Ujenzi wa kanisa, twalazimishwa kutoa.

Verse 6

Kumbuka Ibrahimu, alitoa mwanawe

Kama sadaka kwake Mungu Baba wa mbinguni

Na sisi kwa furaha, tupeleke zawadi

Itakayopendeza, kama ile ya Abeli