Verse 1
Bwana Yesu alituachia amri ya mapendo
Ili tupendane kama yeye alivyotupenda
Tena akasema, akasisitiza,
Mpende jirani, kama nafsi yako
Chorus
{ Mpende - adui yako
Mpende - muombee neema
Mpende - adui yako
Mpende - muombee Baraka } *2
Verse 3
Sisi tulivyoumbwa wanadamu hatulingani
Kwa tabia kwa maisha hata kwa matendo yetu
Wapo wa hekima, wasemao ukweli,
Na wenye kiburi, wasio na busara
Verse 4
Hata ukinyanyaswa jitahidi kuvumilia
Usiwe mwenye ghadhabu ukalipiza kisasi
Ukihuzunishwa, mkimbilie Yesu,
Atakupa faraja, heri na fanaka
Verse 5
Usikumbuke ubaya uliokwisha tendewa,
Hiyo itakuwa njia ya kukaribisha chuki
Ukisha samehe, usahau yote,
Ukatae yote, yasiyo ya hekima