Mpendane Daima
Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Marian,WeddingThanksgiving
Verse 1
Mungu akaona si vyema mtu huyu awe peke yake
Nitamfanyia mwenzake yule wanafanana naye
Akaumba mwanamke, kamleta kwake mwanamume waishi pamoja
Chorus
{ Ewe Bwana - mpokee mke wako tangu leo
Ewe Bibi - mpokee mume wako tangu leo
Muishi nyote pamoja, mpendane daima
Msitengane daima, msivunje agano } *2
Verse 3
Mungu akawapa uwezo watawale viumbe vyote
Mungu akasema zaeni muijaze dunia kwa watu
Baraka za Mungu Baba, zimewashukia tangu leo zaeni matunda
Verse 4
Ewe mwanamume mpende mke wako kwa moyo wote
Nawe mwanamke heshimu mume wako mtii daima,
Ndoa ni maagano, kati ya watu wawili wapendanao
Verse 5
Nyumba yenu iwe hekalu lake Mungu kanisa ndogo
Nyumba ya amani upole na furaha nyumba ya sala
Mungu ameunganisha mwanadamu asitenganishe daima dawamu