Moyo Wangu Wa Utulie
Moyo wangu na utulie kwako Bwana Mungu wangu - na mwokozi wangu
Maana wewe Bwana ndiwe kimbilio langu - tena mlinzi wangu *2
Wewe ndiwe Bwana - wa neema
Fadhili zako - ni za milele
Nikupe nini - Bwana mimi nikushukuru
Umenipa Bwana - na uhai
Pia na nguvu - za kutembea
Nafsi na roho - zangu kweli zimeridhika x2
Asubuhi niamkapo nitalisifu jina lako,
Kwa nyimbo nzuri za furaha mchana mimi nitaimba,
Usiku utimiapo, mimi nitakushukuru,
Kwa maana ninaishi kwa neema zako.
Kila nitembeapo mimi naona utukufu wako,
Wewe waniongoza mimi, kila hatua nipigayo,
Wewe ni Mungu mkuu, na mwenye Baraka tele,
Ninazo sababu tele za kukusifu wewe.
Ewe Bwana unanijua hata ndani ya moyo yangu,
Unaziona siri zangu hata wajua nitakalo,
Ninakuomba ee Bwana, uyajibu maombi yangu,
Kwa kuwa wewe ndiwe tumaini langu
Moyo wangu hukutafuta mchana hata na usiku,
Na mimi ninapokuita kweli wewe huniitika,
Karibu uishi kwangu, nami niwe ndani yako
Usikubali Bwana nitangane na wewe