SectionsExitMoyo Wako Yesu Mpendelevu

Moyo Wako Yesu Mpendelevu

LentExit
Verse 1

Moyo wako Yesu mpendelevu, watuhurumia maskini

Wawapokelea wakosefu kwa msamaha, wema na amani

Moyo wa hazina ya neema utujalie daima *2

Yesu twasalimu wako moyo, twakushukuru kwa mapenziyo

Verse 2

Moyo makimbilio salama, twakujilia japo wadhambi

Tupokee leo kwa huruma, kasikilize yetu maombi

Yesu uturehemie, kwa wema tufanyizie

Twataka kukutii daima, na kwako kupata usalama *2

Verse 3

Moyo ukashibishwa huzuni, kwa kutustahilia msamaha

Pia ukatiwa msalabani, ya Mbingu utupatie Raha

Tufundishe leo pia kukupenda kuzidia donda lako

Utufungulie kwako milele tukimbilie *2