SectionsExitMizinga Maroketi

Mizinga Maroketi

Ordinary TimeExit
Verse 1

Amani ya dunia imetoweka

Tumuombe Mwenyezi aturudishie

Tamaa ubinafsi vilivyoshamiri

Ni sumuyo amani tunayohitaji

Chorus

{

Aa-eh njooni wote

Aa-eh tusali pamoja

Aa-eh tuombee amani

Hatari inatukabili

Tumuombe Mungu atuepushen} * 2

Verse 3

Mizinga maroketi imetayarishwa

Madege ya kutisha ituangamize

Ngao yetu wanyonge ... ...

Yatubidi tusali vita tutashindan

Verse 4

Ujambazi wa kutisha umetuandama

Mali yathaminiwa kuliko uhai

Twahitaji ulinzi wa Mungu Mwenyezi

Aombaye hupewa, njooni tuombe

Verse 5

Ndani ya familia moto unawaka

Kupigwa tusi mateke sasa ndizo sala

Watoto nao pia ni vurugu tupu

Hawana mchungaji kwenye familia

Verse 6

Wito umetolewa tusali rozari

Baba Mtakatifu anatuhimiza

Matendo ya rozari tuyatafakari

Naye Mama wa Mungu atatusikia