Verse 1
Amani ya dunia imetoweka
Tumuombe Mwenyezi aturudishie
Tamaa ubinafsi vilivyoshamiri
Ni sumuyo amani tunayohitaji
Chorus
{
Aa-eh njooni wote
Aa-eh tusali pamoja
Aa-eh tuombee amani
Hatari inatukabili
Tumuombe Mungu atuepushen} * 2
Verse 3
Mizinga maroketi imetayarishwa
Madege ya kutisha ituangamize
Ngao yetu wanyonge ... ...
Yatubidi tusali vita tutashindan
Verse 4
Ujambazi wa kutisha umetuandama
Mali yathaminiwa kuliko uhai
Twahitaji ulinzi wa Mungu Mwenyezi
Aombaye hupewa, njooni tuombe
Verse 5
Ndani ya familia moto unawaka
Kupigwa tusi mateke sasa ndizo sala
Watoto nao pia ni vurugu tupu
Hawana mchungaji kwenye familia
Verse 6
Wito umetolewa tusali rozari
Baba Mtakatifu anatuhimiza
Matendo ya rozari tuyatafakari
Naye Mama wa Mungu atatusikia