SectionsExitMimi Ndimi Baba Yao

Mimi Ndimi Baba Yao

Easter,Easter,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeExit
Chorus

{Mimi ndimi Baba yao Baba milele (milele),nnao ni wanangu Nitawasikiliza nitasikia (mimi),nwakinililia katika taabu} *2

Verse 2

Mimi ndimi wokovu wa watu, nitawaokoa

Wakinililia katika taabu yoyote, nitawasikia

Mimi ndimi aishikaye kweli, nitawahukumu

Walioonewa na taifa lisilo haki, nitawafungua

Verse 3

Mimi ndimi mchungaji mwe-ema, nitawakusanya

Waliotawanyikia nchi za ugenini, nitawarejesha

Mimi ndimi mwa-limu wa watu, nitawafundisha

Waliolemewa na mizigo yao mizito, nitawapumzisha

Verse 4

Mimi ndimi m-kate wa uzima, nitawashibisha

Wote wenye njaa na kiu ya haki hakika, nitawashibisha

Mimi ndimi ufufuo wa kweli, nitawafufua

Wakinirudia na kutubu maasi yao, nitawasamehe

Verse 5

Mimi ndimi kimbilio la watu, nitawahifadhi

Waliotengwa kando na jamaa zao, nitawapokea

Mi-mi ndimi wo-kovu wa watu, nitawaokoa

Wakinililia katika taabu yoyote, nitawasikia