Verse 1
Mfalme wa amani mpeni heshima,
Yerusalem mjini anaingia
Na unyenyekeo na upole mkuu
Anapanda punda Mwana wa Mungu.
Chorus
Hosana juu, hosana Juu, hosana juu.
Verse 3
Njooni Mahebruni, njooni watoto,
Leteni matawi ya kumsalimu.
Mwana wa Daudi kweli Masiya
Anakuja kwenu mwenye huruma.
Verse 4
Tandikeni nguo miguuni pake,
Imbeni zaburi, shangilieni.
Mbarikiwa huyu ajaye kwetu
Kwa Jina la Bwana Mkombozi mkuu.
Verse 5
Ufurahi sana, we` Yerusalem
Yule wamwabudu roho za mbingu.
Na huruma pale anakujia,
Haki na amani akuletea.
Verse 6
Ndimi za wachanga zafumbulia,
Kwa mwujiza sifa yake Masiya
Na makundi yote ya malaika
Sifa na heshima wanamtolea.