SectionsEntranceMbona Mwafurahi

Mbona Mwafurahi

Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary Time,Ordinary TimeEntrance
Verse 1

Mbona mwafurahi, (leo) sisi tuna amani (kweli)

Mbona mwafurahi, (leo) sisi tuna upendo (kweli)

Chorus

{ Yesu ni mwalimu (kweli), tena ni dereva (wetu)

Akiwa usukani sisi tuko salama } *2

Verse 3

M-nakwenda wapi, (kule) nyumbani mwake Bwana

Leo kuna nini, (ili) tutoe shukrani (zetu)

Verse 4

Njooni watu wote, (leo) tukamwimbie Mungu

Njooni tusujudu, (humu) hekaluni- mwake

Verse 5

Mwili wake Bwana, (ni) chakula cha roho (zetu)

Damu yake Bwana, (ni) kinywaji cha- kweli (kweli)

Verse 6

Tufanyeni shangwe, viumbe wake Mungu (Baba)

Kwa vigelegele, (pia) kwa kupiga makofi (sana)