Baada ya kuteswa na kusulubiwshwa msalabani
Aliona walichokifanya hawakukijua
Aliwaombea kwa Mungu akisema
Baba uwasamehe hawalijui wanalofanya
Kulikuwa mhalifu liyemtambua kuwa yeye ni Mungu
Alitubu akaambiwa
Nakuambia hakika leo, utakuwa pamoja nami peponi
Alitukabidhi kwa mama yake
Na huyo ndiyo mwombezi wetu aliposema
Mama tazama huyu ndiye mwanao
Tazama huyu ndiye mamako
Aliona kiu baada ya mateso makali
Hadi alisema mwenyewe naona kiu
Baada ya mateso makali hayo
Aliyoteswa kwa ajili ya dhambi zetu
Aliona yote aliyotumwa na Mungu kuwa yametimia
Aliposema Yametimia *2
Ndipo alipolia kwa uchungu na kumbwambia Baba
Eloi eloi lamasabakidani, Mungu wangu Mbona umeniacha
Mwisho kabisa aliikabidhi roho yake kwa Baba
Akisema Baba mikononi mwako Naiweka Roho yangu