SectionsEntranceMalaika Kaleta Noeli

Malaika Kaleta Noeli

ChristmasEntrance
Verse 1

Malaika kaleta Noeli ya kwanza,

Kwa wachunga kondoo katika makonde,

Bethlehemu wakawa walinzi wa zamu,

Wakaona usiku ajabu ya nuru

Chorus

{ Noeli, Noeli, Noeli, Noeli,

Yesu yu Mungu na binadamu } *2

Verse 3

Wakaona mbinguni, mwangaza wa nyota,

Ing'aayo kwa mbali na masharikini,

Wakaenda upesi, walivyoambiwa.

Bethlehemu wamwone Mwokozi horini

Verse 4

Mashariki watoka wafalme watatu,

Mamajusi waliotafuta mfalme,

Wafuata hii nyota waliyoiona,

Wasipate kumkosa wanayemtafuta

Verse 5

Kiongozi ni nyota iliyowaleta

Hata mji wa Daudi alimozaliwa

Ikakaa mara moja isiendelee

Pale pale nyumbani alimo Mwokozi

Verse 6

Mamajusi walipoingia nyumbani

Wakapiga magoti kwa heshima kuu

Mara hiyo walipozifungua hazina

Manemane, uvumba, dhahabu, watoa

Verse 7

Basi sisi wakristu na tumsujudie

Tumhimidi Mwokozi, aliyeviumba

Vitu vyote mbinguni duniani na sisi

Na ametufia na kutukomboa